Mamlaka ya mapato Tanzania TRA Zanzibar yaleta mabadiliko ya nyaraka

  Mamlaka ya mapato Tanzania TRA Zanzibar  imesema imebadili mfumo wake wa sasa wa kuhifadhi kumbu kumbu za walipa kodi na kuweka mfumo wa kisasa unaoendana na ukuaji wa teknolojia.
Saleh Haji Pandu
   Akizungumza na mwanahabari wetu afisa elimu kwa mlipa kodi wa mamlaka hiyo Saleh Haji Pandu amesema wameamua kuandaa mkakati maalum kwa wafanya biashara na kuhakiki  taarifa zao kwa kumjua mlipa kodi yupo maeneo Fulani anayofanyia biashara.

   Amesema ni vyema kwa  wafanya biashara wenye TIN kuboresha au kuhakiki taarifa katika ofisi za mkoa na wenye TIN zisizo za biashara kuhakiki taarifa zao katika ofisi yoyote ya TRA.     
 Akizungumzia ongezeko la watu wanaofanya biashara katika maeneo yasiyokuwa rasmi na kutolipa kodi,amesema hali hiyo inaipa mzigo Serikali katika kuendesha huduma za jamii na kutotimiza lengo walilokusudia.


Aidha ameitaka jamii kuwa na uzalendo wa kusajili biasha zao ili kuona mamlaka hiyo inafikia lengo hasa la kufanikisha matarajio yao ya kuwepo kwao na kuwata wananchi kudai risiti. 

Previous
Next Post »

Ads