Wakulima wa mbogamboga na matunda wahamasishwa kujiunga na vikundi vya ushirika

   

Waziri wa kilimo mali asili  mifugo na uvuvi Zanzibar Hamad Rashid amewataka wakulima wa kilimo cha mbogamboga na matunda kujiunga na vikundi vya ushirika ili kunufaika na huduma ya mikopo inayotolewa kwa lengo la kuboresha maendeleo katika  kilimo wanchozalisha.
   Akizungumza na mbwanajr huko ofisini kwake maruhubi amesema wafanya biashara wengi wakiwemo wakulima wa mbogamboga wanafanya biashara kinyume na utaratibu jambo ambalo linapekekea kutotambuliwa kisheria na kukuso huduma ya kupatiwa mikopo.
   Hata hivyo amesema wakulima wanapojikusanya pamoja na kubuni njia bora za kuimarisha maendeleo ya kilimo itarahisisha upatikanaji wa kupatia mikopo kwa wakati na kuingia katika kilimo cha biahara kwa lengo la kujikombowa na umaskini na kukuza uchumi wa nchi.
    Aidha ametowa wito kwa wakulima kuzitumia taasisi za fedha katika shughuli zao za kilimo ili kurahisisha kutambuliwa kisheria wakati wa kupatiwa mahitaji muhimu kazi kazi zao.
   Zaidi vikundi kumi na sita ikiwemo zimepatiwa mikopo ya kujiendeleza na kilimo ili kufikia kilimo cha bishara.
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video zote kali kutoka mbwanajr !
Previous
Next Post »

Ads