Mchezaji wa klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ujerumani azungumzia umuhimu wake wa kuwa na imani ya dini ya Kiislamu.

Mchezaji wa klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ujerumani, Shkodran Mustafi amezungumzia umuhimu wake wa kuwa na imani ya dini ya Kiislamu.
mustafi-shirt-1024x643
Nyota huyo mwenye asili ya Albania, ambaye anacheza nafasi ya beki wa kati na pembeni mwenye umri wa miaka 24 hivi karibuni alifanya mahojiano na gazeti la The Sun na kubainisha umuhimu wa kuwa na imani ya dini ya Kiislamu.
Alisema nia yake ya kutaka kutekeleza ibada ya Hijjah, akisema, “Uislamu ni muhimu kwangu kuliko kila kitu.”
Mustafi pia alisema hupata ugumu wakati mwingine katika jitihada za utekelezaji wa baadhi ya ibada za Kiislamu hasa katika mwezi mtukufu wa Ramadhan kutokana na uchezaji.
9456947
“Najivunia na kufurahia kuwa Muislamu. Siku moja nitatekeleza ibada ya Hijjah ambayo tunatakiwa kutimiza angalau mara moja maishani na hilo ndilo lengo langu kuu.”

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia kwa ku like FacebookTwitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga naYoutube kuangalia video zote kali kutoka mbwanajr !

Previous
Next Post »

Ads