Omba Omba marufuku Mkoa wa mjini magharibi


Ofisi ya  mkuu wa  mkoa mjini magharib  imekataza rasimi  mtu yoyote katika  maeneo yoyote kufanya kazi ya omba omba katika mkoa wa mjini magharib hali inayosababisha kuondoa haiba ya muonekano wa Nchi hasa kwa wageni.
Akizungumza na maafisa kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashataka pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama huko ofisi kwake Vuga amesema katika mkoa huo kumekithiri vitendo vya omba omba vinavyofanywa na watu wa rika tafauti wakiwemo wazee vijana na watoto katika maeneo mabilimbali yakiwemo madukani, maofsini na mitaani.

Akilitolea ufumbuzi suala la uzuzuraji wa wanyama wakiwemo ngombe, punda na wengineo ambao lilipigiwa marufuku hivi karibuni  katika maeneo ya  mjini na baadhi ya maeneo ya magharib amesema 
Ayoub amesema  katika kuhakikisha omba omba wanaondoka katika mkoa huo tayari mikakati imeshakamilika kutoka vyombo vya ulinzi na usalama.
Akizungumza na mbwanajr blog mmoja ya omba omba hao hakutaka jinalake kutajwa katika mtandao huu wa  habari  amesema ameamua kujiingiza katika kazi hiyo kutokana na hali ngumu ya kimaisha.
Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara wamesema wanasikitishwa na kazi hiyo inayofanywa na baadhi ya watu kwa kupita madukani pamoja na kufanya makazi yao katika maeneo ya madukani hali inayopelekea kero katika maeneo hayo.
Mmoja wa wafanyabiashara hao Said Salehe mfanyabiasha wa bidhaa za ujasiriamali hivyo ameishauri serikali kuandaa mbinu mbadala za kiwasaidia zitakazowezesha kuondoakana na tabia hiyo 
Previous
Next Post »

Ads