Wanafunzi wahimizwa kutumia Mitandao

   

 Wanafunzi wa vyuo vikuu wamehimizwa kutumia taaluma zao katika kubuni mbinu za kujiajiri kwa lengo la  kujikwamua na umaskini na kuondokana na utegemezi wa ajira serikalini.
   Akifunga mafunzo ya siku mbili kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali juu ya utengezeji wa picha mitandaoni muhadhir kutoka chuo cha Abdul rahman sumait Mohammed Saleh Muhammed amesema wanafunzi wa vyuo wakiitumia ipasavyo elimu walionayo itasaidi kuleta maendeo ya kiuchumi.
   Aidha amesema baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakikaamitaani baada masomo yao ya vyuo na ya mafunzo walioyapata jambo ambalo husababisha kushindwa kutimiza malengo yao na kupelekea wimbi kubwa la vijana wasiokuwa na ajira.
  Wakizungumza na zenj fm radio nnje ya mafunzo hayo baadhi ya wanafunzi wametowa wito kwa wanafunzi wenzao kuyatumia ipasavyo mafuzo waliyapata kwa lengo la kukuza taaluma yao katika kuimarisha uchumi na maendeleo ya Nchini.

   Zaidi ya wananfunzi 50 kutoka vyuo mbalimbali vya Zanzibar ikiwemo Suna,Ipa,Zifa na Ispc yenye lengo la kuwaandaa wanafunzi wa vyuo kubuni mbinu za kujiajiri wanapo maliza masomo. 
Previous
Next Post »

Ads