Siku ya wazee dunia Zanzibar

                      Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Shein ametaka kuwajibishwa watendaji wa serikali waliowaingiza wazee wasiokuwa na sifa kwenye orodha ya malipo ya pencheni.
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani uwanja wa Gombani Pemba ameitaka Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto kuwatafuta watumishi hao na kuwajibisha.
Amesema anazo taarifa ya kuwepo baadhi ya wazee waliorozeshwa kwenye urodha ya malipo hawajatimiza miaka 70 jambo ambalo linakwenda na utaratibu uliokusudiwa.
Dk. Shein pia amesema amesema wazee wenye sifa waliostahili kuingizwa kwenye daftari la malipo lakini hawakupewa fursa hiyo na kuiagiza Wizara hiyo kuwatambua watu hao.
Wakizungumza na mwandishi wetu  nje ya madhimisho hayo baadhi ya wameiomba serikali kundaa utaratibu wa kuwapatia huduma za afya na matibabu kutokana na wengi wao hawana uwezo.
Madhimisho ya Siku ya Wazee Duniani huadhimishwa kila ifikapo tarehe 1 Oktoba kila mwaka, na kwa Zanzibar mwaka huu maadhimisho hayo yamefanyika kisiwani Pemba.









Madaktari Bingwa kutoka hospitali ya rufaa ya Muhimbili waliendesha kazi za upimaji wa afya kwa wazee wa mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni moja ya maadhimisho ya siku ya wazee duniani hapo.
        Upimaji huo wa afya umeendeshwa chini ya udhamini wa Jumuiya ya kuwasaidia watu wenye matatizo Baps Charitable na kuanyika katika kjiji cha Paje wilaya ya Kusini.
        Naibu katibu mkuu wizara ya Kazi, Uwezeshaji, wazee, vijana na wanawake Mauwa Makame Rajab jamii kuheshimu haki za wazee.
        Amesema vitendo vya ukatili wanaofanyiwa wazee ikiwemo mauwaji na kuwadhalilisha kijinsia ni kukiuka misingi ya haki za binadamu, hivyo serikali haitakubali kuona vitendo hivyo vinaendelea.
        Baadhi ya wazee waliopata huduma za matibabu wameziomba taasisi nyengine kusaidia huduma za afya kwa kundi hilo kutokana na wengi wao hawana uwezo.
        Uchunguzi huo wa afya kwa wazee ulifanyika kwa maradhi ya meno, masikio, shindikizo la damu, malaria, kisukari huku wazee zaidi ya 300 wamejitokeza kufanyiwa uchunguzi huo.
Previous
Next Post »

Ads